Katika Agano Jipya, kuna barua 21 au nyaraka zilizoandikwa na viongozi wa Kikristo wa mwanzoni kwenda katika jumuiya za wafuasi wa Yesu zilizokuwa katika ulimwengu wa kale wa himaya ya Roma. Kusoma kwa hekima barua hizi kunahusisha kujifunza kuhusu muktadha wake wa kihistoria. Barua hizo ziliandikwa kwa akina nani, wapokea barua hizi waliishi wapi, na ni nini kilichochochea kutuma barua hiyo? Katika video hii, tunachunguza safu tofauti za muktadha wa kihistoria kwa kutumia barua hizi ili tuweze kuelewa vyema hekima zinazotoa leo hii.
#bibleproject #Biblia #nameofvideo