Mpendwa tunaendelea na somo letu ,ambapo tunakaribia kumaliza aya ya 5.Na
kwa sasa ningependa niseme somo hili limekuwa la kuridhisha na la kufahamisha
mengi.
Heri waliosamehewa makosa yao,na waliositiriwa dhambi zao.Heri mtu Yule ambaye Bwana hamhesabii dhambi.Je? uheri huo ni kwa waliotahiriwa , au kwa hao pia
wasiotahiriwa?Kwa kuwa twanena ya kwamba kwake Ibrahimu Imani yake
ilihesabiwa kuwa ni haki.Alihesabiwaje basi?
Kwenye kipindi kilichopita tuliongelea pakubwa kuhusu jinsi ya kuishi maisha ya ukristo.Na jinsi ilivo ada ya kipindi hiki nitakusomea kwa muhtasari aya tulizonukuu kwenye somo lililopita.