Makanisa mengi karibu yote huonyesha na kuanika yote wazi msalaba maana katika Imani na mafundisho ya ukristo msalaba ni lazima. Warumi walitumia msalba kuwatesa na kuhukumu waasi. Sisi wakristo huzingatia na kuhimiza ujumbe na somo la msalaba. Somo na ujumbe wa kuteswa kwake bwana wetu yesu kristo msalabani kwa sababu ya makossa na dhambi zetu. Ilikuwa muhimu kristo afe msalabani kwaajili na kwasabau yetu sisi wenye dhambi
Katika maisha yetu tunavyo vitu tunavyothamini kuliko vingine kulingana na umuhimu wa vitu vile katika maisha yetu. Hii ni baada ya uchunguzi na upelelezi wa kina sana na hivyo basi mtu aweza kuwa na Imani na kile chombo au kituLakini hapa Paulo atufunza Imani ilivyo maana Zaidi
Baadhi yetu hufikiria ya kwamba Imani yetu ni kikwazo wengine hufikiria na kuwaza waza kuwa Imani ni hali ya akili tu lakini tukubali ya kwamba maisha yetu na uammuzi wetu hutegemea namna ya Imani ilivyo na nguvu na uweza wa kuyatenda mabo ya ajabu kwa utukufu wake mungu. twahitaji mazoea ya Imani anza kujifunza kujiombea kwa Imani maana hata kabal ya kuomba mahitaji yetu tayari anayajua n ahata majibu na sulihisho zimo na hutoka kwake mugnu wetu maana hata roho mtakatifu wa mungu hutuombea na kutusaidia katika udhahifu wetu kwa maana hatujui kwamba jinsi itupasavyu lakini roho mwemyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa. Yeye aichungizaye mioyo aijua nia na roho iliyo kwa kuwa huwaombea watakatifu kama apendavyo mungu.
Kwanini ibrahimu alijulikana sana katika historia ya biblia? Jibu ni kwamba ibrahimu alikuwa mtu wa vitendo na mtu wa Imani na ndiye baba yetu. Lakini mtume Paulo amwonaje ibrahimu?
Baba yetu ibrahimu ni mtu muhimu na wa maana katika mpango wa mungu kwetu na katika hitoria inayoonyesha namna mungu alidumisha uwepo wake kwa ibrahimu ni muhumu na tunayo sababu ya kujua na kufahamu ukweli wa agano katia ya mungu na ibrahimu. Hata yesu mwenyewe aliyazungumzia hayo katika vitabu vya injili